Posts

RIWAYA:: MAISHA YANGU YA UVUVI SEHEMU YA ISHIRINI NA NNE 24

Image
ENDELEA.....................  .................  ...24.........  Salha alitulia kisha akaniuliza tena,  "Mnali, unajua sijakuelewa japo umenieleza kila kitu kinachokuhusu, sasa inawezekana vipi usile chakula cha kawaida alafu badala yake ukapenda nyama mbichi?".  Swali lake lilikuwa lina maana kubwa sana kwangu lakini sikuwa na namna zaidi ya kuwa muwazi mbele yake.  "Salha! Nisikilize kwa makini tena kwa umakini mkubwa sana"  "Ndio nakusikiliza".  Niliinuka kisha nikauelekea mlango nikautikisa ili kujua kama umefungwa na kweli ulikuwa umefungwa.  "Vipi! Hakuna mtu tofauti na mimi na yule mlinzi"  "Kwa nini uishi peke yako"  "Basi tu haya tuendeleee"  "Sawa Salha! Kama nilivyokuelekeza natafutwa na makundi mawili mpaka sasa tena matatu..hapa ninapokuambia polisi nao wananitafuta, maisha yangu ni ya ajabu sana na yameibuka kutoka hivyo na tatizo ni Uvuvi wangu".  "Uvuvi wako? Kivipi tena".  Aliuliza  "M...

RIWAYA:: MAISHA YANGU YA UVUVI SEHEMU YA ISHIRINI NA TATU 23

Image
ENDELEA........  .................  .................  ................  ................Baada ya kuhakikisha kuwa nilikuwa kwenye njozi nilikaa kitako lakini bado harufu kali ilizidi kunibana puani mwangu.  Siku na hata la kufanya kwani mwanga ule wa mwanzo sikuupata tena zaidi ya kiza kinene kutanda.  Hata njia ile ya mwanzo niliyoingilia sikuweza kuiona tena, hapo ndipo nilipojua kuwa sasa nakwenda kuangamia. Nyakati hizo nilijishangaa ule unyamaunyama ulishaniisha kabisa na nikabaki kuwa wa kawaida sana. Nilisimama kisha nikaanza kuchunguza mazingira ambayo ningeweza kutoka mule pangoni.  Kwa kweli nilijiona nakwenda kufa kwani hewa yote ya oxygen ilikuwa imepotea. Nilijipa moyo kwa kutembea kwenye miili ya wanyama waliokufa.  Nilipata wakati mgumu kupitia ile ndoto kuwa lile sanduku ndio maisha yangu na nahitajika nifanye harakati zote kulipata, lakini hawa wasifahamu kuwa natoka.  Niliendelea kuzunguka mpaka pale nilipoishiwa nguvu za k...

RIWAYA:: MAISHA YANGU YA UVUVI SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI 22

Image
ENDELEA......  .................Nilikaa kwa takribani dakika kadhaa, jua likapambazuka na asubuhi ndio inaingia. Watu walianza kuingia maeneo yale ya ufukwe ndipo wakaanza kuzunguka lile eneo huku wengine wakawa wanakimbia ovyo.  Akili yangu ilirejea sasa kwa kile kilichotokea kuwa mimi ndio sababu kubwa.  Niliwaza baada ya kuwa na akili ya kawaida sasa ya kibinaadamu na kujua kuwa yale niliyoyafanya si mazuri kabisa. Ila tatizo nilishindwa kurudi pale kuwa watanifikiria vipi. Nilisukuma lile jahazi langu taratiibu kuelekea pale ufukweni.  Nikiwa na bukta yangu, nilikaribia fukwe ndipo watu wakaanza kugeuka na kunitizama mimi pale. Tukawa sasa tunashangaana. Lile eneo wengi walikuwepo akiwa na yule mzee mashuhuri kwa mambo ya uvuvi, yeye alikuwa ananifahamu fika kutokana na kuujua mkasa wangu kidogo.  Mimi pia macho yangu yaligota kwenye viini vya macho ya yule mzee na kufanya tutizamane kwa sekunde kadhaa. Palepale lilisikika gari lenye mlio wa king'ola kuhashi...

RIWAYA:: MAISHA YANGU YA UVUVI SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA 21

Image
ENDELEA.......  .......Mlango unafunguliwa na kuingia Vijana kama watatu ambao sikuwa nawafahamu kwa sura, bali kwa idadi kutokana na wao walikuwa wakinimulika tochi usoni na kufanya nikose nuru.  "Eheee! Kwa hiyo bwana Paul hakuona vijana wa kufanya nao kazi hatari kama hii na wakakutumia wewe?".  Mmoja wao aliongea aliyeonekana kuwa kama mkubwa kati ya wale watatu. Lile swali halikunifanya nijibu kwa haraka kama vile ambavyo wao walihitaji nijibu bali nilibaki kuwa kimya. Hii yote kutokana na kichwa changu kupokea maumivu makali ambayo yalisababishwa na purukushani za kutwa nzima hadi nyakati zile.  "Kijana! Sisi hatuna shida na wewe kabisa, tunachohitaji ni kujua unaeje huyu bwana Paul?"  "Mimi sijui chochote".  Nilimjibu.  Lakini ilionyesha wazi kuwa jibu langu hakulizika nalo maana alisimama kisha akainama tena na kuniangalia  "Unasemaje?"  Aliniuliza swali lilelile  "Mimi sijui chochote"  Alinizaba kibao cha maana, kilichonipe...

RIWAYA:: MAISHA YANGU Y UVUVI SEHEMU YA KUMI NA TISA 19

Image
ENDELEA...........  .......Safari ile sikuwa nafahamu napelekwa wapi, kwa kuwa nilikuwa sijifahamu kabisa, hii ilitokana na mwili wangu kukosa nguvu baada ya lile tukio kunitokea kwa wakati mfupi kama ule na kupotea ghafla. Ilinichukua muda sana mpaka hali yangu kurudi kutoka kwenye usingizi mzito wa nusu kifo, Nilishtuka baada ya kuhisi ubaridi mkali mwilini mwangu, ndipo nilipoangalia macho yangu baada ya kugundua kuwa sipo sehemu salama. Kilichonijulisha kuwa sipo sehemu salama ni baada ya kuzisikia kelele za watu wakicheka kwa kebehi ya aina yake.   "Niko wapi hapa mimi"  Nilijiuliza mwenyewe bila hata ya kupata jibu. Niligeuza shingo yangu sehemu mbalimbali za ile nyumba ndipo nikakutana uso kwa uso na bwana Paul. Nilishtuka sana, kwani sikutegemea kama yule mzee atanileta sehemu kama hii.  "Mnali?"  Paul alniita  Nilimuangalia tu bila kuitikia  "Unajisikiaje kuwa maeneo haya?"  Paul aliniuliza.  Pia hata hilo sikuweza kumjibu....

RIWAYA:: MAISHA YANGU YA UVUVI SEHEMU YA KUMI NA NANE 18

Image
ENDELEA.........  .......Kwa kuwa bwana Mjumbe nilimuona akiwa mbishi kama pilipili yenye kuwasha mdomoni pindi inapoliwa. Niliondoka na kumuacha akiwa ananiangalia huku akinisindikiaza kwa kauli ileile ya awali ambayo nilipata kuisikia kwa umakini zaidi ya awali."Wewe kijana huu mtaa utakushinda kabisaa kwa hali hiyoo na kiburi hiko ndicho kilimfanya Kibona aweze kufa". Nilitamani kusimama lakini nikabakia kusikitika kwa nafsi yangu pamoja na mwili wangu kuusongesha mbele kwa kutohitaji swala lolote baya.  Nimeshafika hadi nyumbani nafanya nini hali ya kuwa hakuna chochote kilichomo ndani, nabaki kuduwaa na wakati nazidi kuduwaa ndipo nashtuka kushikwa na mtu akiwa nyuma yangu hakuwa mwingine bali ni yule mzee ambae aliniunganishia dili kwa bwana Paul, "khaaa! Mnali, achaa weeee haya mbona maajabu". Nilimuangalia sana huku nikimshangaa "maajabu kivipi?" Nilimuuliza swali. "Wewe huoni kama unazidi kuishangaza dunia haya umeponapona vipi huko baharini!...

RIWAYA: MAISHA YANGU YA UVUVI SEHEMU YA KUMI NA SABA 17

Image
ENDELEA……..  Baada ya Salha kuamka alinikuta mimi nikiwa kwenye utupu wangu nikimkodolea macho kama panya aliyebanwa na mlango. Sikuwa mtu wa kawaida kabisa kama inavyotakiwa kwa wengine kwani nilijihisi kama mnyama kabisa. ‘Mnali unatakla nini naa! Mbona uko hivyo sasa’ alikuwa anaongea lakini sikuwa namsikiliza kabisa nilichofanya ni kuendelea kuushikilia ule mguu wake na mimi nikiwa kwenye hali mbaya ya kutaka kumuingilia kimwili dada wa watu.  Mpaka dakika kadhaa zilizopita hakika nilifanikiwa kumvamia na kumsaula kila kitu, lakini kwa upande wake hakuonyesha pingamizi yeyote kwangu Zaidi ya kugugumia kama mtu ambae anaonea hali kuwa anajua nini kinataka kuendelea na yeye ndie mhanga mkuu. Mpaka muda wa dakika kama kumi tayari nilishaweza kuingia langoni mwa dada Salha na kumfanya yeye akihemea juu juu. Kutokana na mwili wangu kuchemka damu kwa kasi sana misuli yangu ya kila eneo hasa ile ya kiumeni iliweza kusimama barabara mpaka Salha alilalama Zaidi.  Nakumbuka nil...