Mgonjwa wa Corona Aliyefariki KENYA Alikuwa na Kisukari



Raia wa Kenya aliyeaga dunia siku ya Alhamisi nyakati za mchana katika chumba cha wagonjwa mahututi hospitali ya Agha Khan jini nairobi ambako alikua amelazwa alikuwa anaugonjwa wa kisukari. 

Raia huyo mwenye umri wa miaka 66, alikuwa amewasili nchini Kenya tarehe 13 mwezi Machi kutoka Afrika Kusini kupitia Swaziland. 

Katika taarifa iliotiwa saini na waziri wa Afya Mutahi Kagwe, serikali ilisema kwamba ilipokea kwa huzuni habari za kifo cha Mkenya huyo ambaye alikuwa amekutwa na virusi hivyo baada ya kupimwa.] 

Mbowe ajiweka karantini na familia yake 
Katika mkutano na wanahabari afisa mkuu katika wizara ya afya Mercy Mwangangi alisema kwamba visa vyote vya hivi karibuni ni vya Wakenya waliokaribiana na watu walioripotiwa kuwa na ugonjwa huo hapo awali. 

Rais Uhuru Kenyatta alitangaza hatua kadhaa ambazo alisema zitasaidia serikali yake kukabili janga la corona ikiwa ni pamoja na amri ya kutotoka nje kuanzia Ijumaa Machi 27 kuanzia saa moja usiku hadi saa kumi na mbili asubuhi.

Comments

Popular posts from this blog

SMS 47 ZA MAPENZI ZITAKAZO MNYEGEZA** MPENZI WAKO

KWANINI WADADA WENGI WAREMBO NA WANAOJIONA WAREMBO HUCHELEWA KUOLEWA,HUKOSEA KUOLEWA AU KUTOOLEWA KABISA?SOMA HAPA

HATUA ZA KUCHEZEA KIHARAGE NA KISIMI