Posts

Showing posts from November, 2019

SEX MACHINE - SEHEMU YA 09

Image
"Nimechanganyikiwa Maida na ndiyo maana nipo hapa kwa ajili moja tu ya kukuuwa." Alisema Salome na kumfanya Maida ashangae na kuangua kicheko kabisa.  "Hee! Hivi umechanganyikiwa wewe yaani huoni hata haya eti, niko hapa kwa ajili ya kukuuwa (akabana pua yake kwa vidole viwili na kuifanya sauti itokekee nyembamba ya dhihaka), yaani wewe uniuwe mimi?"  "Kwaiyo unashangaa kuwa mimi siwezi kukuuwa au kinachokushangaza ni nini, ngoja uone vile nitakufanyia sasa!" Alisema Salome wakati huo akiwa tayari ameshamsogelea Maida karibu.  "Siwezi kukuacha Maida, mimi moyo wangu kwa sasa hauna amani sababu yako. Umeninyang'anya furaha yangu, siwezi kuishi kwa namna hiyo. Chriss hataki hata kuniona mimi sababu yako?" Aliongea kwa uchungu mkubwa sana Salome. Maida alimtazama binti huyo kwa dharau kubwa kisha akatazama pembeni akasema;  "Nilidhani labda leo umewekwa style ya mbuzi kagoma kwenda ndiyo umekuja kunihadithia kama kawaida yako kumbe limekush

MAPENZI Shida Jamani…Mwanaume Ajinyonga Baada ya Kumkosa Mkewe Kitandani

Image
Mwanaume mmoja mkoani Rukwa amejinyonga kwa kutumia kamba ya nailoni baada ya kugundua mkewe ametoroka usiku na kwenda kwa mwanaume mwingine. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Justine Masejo amesema mnamo novemba 26, 2019 saa 6 usiku, mwanaume iliyefahamika kwa jina la Rafael Leonard (49) mkazi wa kijiji cha Bumanda wilayani Nkasi, alijinyonga chumbani kwake kwa kamba ya nailoni. Amesema kabla ya kujinyonga alikuwa amelala na mkewe, aliposhtuka usingizini alikuta mke wake ametoroka na kwenda kwa mwanaume mwingine ndipo alipokasirika na kupatwa na wivu wa kimapenzi na kuamua kujinyonga. katika tukio jingine, Novemba 23 wilayani humo, watu wawili waliofahamika kwa majina ya Japhet Jelazi (25) na Peter Silunde (8) walipoteza maisha baada ya kupigwa na radi wakiwa wamejikinga mvua chini ya mti. Aidha kamanda huyo ametoa wito kwa wananchi kuwa waangalifu katika kipindi hiki cha mvua za masika ili kujiepusha  na madhara yanayoweza kujitokeza.

SEX MACHINE - SEHEMU YA 08

Image
Sauti ya kugongwa kwa mlango ndiyo iliyomshtua Suzane ambaye alikuwa mezani akijipati chakula cha usiku. Akaamka na kuelekea mlangoni kabla ya kufungua mlango kwanza alichungulia kwenye kijitundu kidogo kinachoruhusu kumuona mtu aliyeko nje kisha akaufungua mlango huo. Tabasamu pana likiwa usoni mwake.  "Karibu sana Chriss, karibu ndani." Alikaribisha.  "Asante madam habari za hapa?" Alijibu salamu Chriss na kusalimia.  "Za hapa nzuri sijui za huko utokako?"  "Za huko ni nzuri pia," alijibu na kuingia ndani, Suzane aliufunga mlango kwa komeo kabisa na kumpita kijana huyo akiwa amesimama. Akasema; "Karibu ukae tupate kwanza chakula cha usiku pamoja kisha ndiyo urudi nyumbani?"  "Ooh! No, madam Suzane. Nyumbani nimecha kula nikaona nije kwanza nikufikishie huu uju...!" Alisema Chriss hata hivyo hakufika mwisho wa sentensi yake, Suzane akamuwahi.  "Najua Chriss lakini sitapenda uondoke hivi hivi bila kupata chochote kitu,

SEX MACHINE - SEHEMU YA 07

Image
"Joesan! Usitake kuniambia hujui. Yule ni kijana wako na anakusikiliza sana acha huko kukuheshimu, sidhani kama ukimwambia kuwa unajambo la msingi unataka kumueleza, anaweza kukukatalia. Hakikisha unaongea naye mambo mazuri na kila ulichomuahidi sasa kinakwenda kutimia na wewe mwenyewe unajua Joesan kuwa anakwenda kuiingizia kampuni mamilioni ya mapesa lakini hata yeye ataingiza pesa nyingi zitakazo badilisha maisha yake kwa kazi hiyo."  "Ndiyo najua," akadakia Joesan na kisha mwanadada huyo akaendelea.  "Sasa, anakwenda kuwa milionea. Hakuna mtu anayekataa pesa lazima ukimueleza hili atakubali hawezi kukataa hata kidogo."  "Hata hivyo sina hakika kama Chriss anaweza kukubali kirahisi, huyu ni kijana mbishi sana kuelewa," akasema Joesan.  "Joesaan!" aliita binti huyo na kuendelea.  "... si wewe wala mimi atakayembadilisha Chriss. Chriss atabadilishwa na Sex Machine Controller (SMC). Hii ndiyo itakayobadilisha maisha yake n

SEX MACHINE - SEHEMU YA 06

Image
SEHEMU YA 06  Alinyanyuka Joesan na kutoka mule ndani ikiwa sasa imetimu saa 05:30 za jioni. Alikwenda hadi bustanini na kujituliza pembezoni kabisa mwa bwawa la kuogelea. Nina muda mrefu sana sijafika mahala hapa, kazi hizi zinanifanya kuwa ubize mkubwa kila wakati. Akawaza Joesan akiwa hapo bustanini akiyashangaa mandhari yake. Leo imenilazimu kufika hapa bila kutarajia mawazo yamenizidi sana sielewi nifanye nini mimi. Aliwaza tena bwana huyo akiwa sasa amesimama ndani ya ile bustani ya maua. Baada ya muda akahisi mikono laini ikimkumbatia kutokea nyuma na kukipapasa kifua chake kilichochanika kutokana na mazoezi mazito.  "Mume wangu leo ni maajabu sana kufika mahali hapa, si kawaida yako maana hata chakula umegoma kula leo, nini kimekupata my dear?" Sauti mwororo ya Martha ikasikika kutokea nyuma ikimuuliza kwa utaratibu mkubwa.  "Hapana mke wangu ni u-bize tu wa kazi hakuna kitu kingine," akazungumza Joesan. Martha alizunguuka kwa mbele na kumtazama vizuri mum