Posts

Mwakinyo Aapa Kuua Leo, Mfilipino Aanza Visingizio

Image
BONDIA wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo ameapa kuwa atahakikisha mpinzani wake, Arnel Tinampay raia wa Ufilipino ‘anafia’ ulingoni huku Mfilipino huyo akiomba waamuzi wasifanye upendeleo. Leo Ijumaa mbele ya Waziri Mkuu wa Tanzania, Majaliwa Kassim ambaye atakuwa mgeni rasmi katika pambano hilo la kimataifa litakalokuwa la raundi 10 litapigwa kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar. Mwakinyo alitoa kauli hiyo ya kibabe wakati wa kupima  uzito jana kwenye kituo cha Azam Media, ambapo alisema kuwa atahakikisha mpinzani huyo hamalizi raundi tano na ikiwezekana kummalizia ulingoni kwenye pambano hilo kutokana na maandalizi makali aliyoyafanya. “Binafsi nimejiandaa vizuri kwa kuhakikisha nashinda kwa ushindi mkubwa hapo kesho (leo Ijumaa) kwa kuwa naamini nimefanya maandalizi ya kutosha,” alisema Mwakinyo. Upande wa Tinampay ambaye anatoka kwenye kambi ya bondia maarufu, Manny Pacquao, alisema amekuja nchini kwa kazi moja ya kuhakikisha anamshinda Mwakiny...

Rosa Ree na Awilo Longomba Katika NYIMBO Moja….Nini Kitatokea?

Image
Inavyoonekana Kuna kitu kinaendelea kati ya Msanii Awilo Longomba na Rapper Rosa Ree Baada ya Leo Wote Wawili katika page zao kupost picha wakiwa Pamoja….Bado hajajulikana ni wapi wamekutana au nini wanatarajia kufanya….lakini tumemcheki Rosa Ree Leo Amesema tusubiri tusiwe na haraka yupo katika kuandaaa vitu vizuri kwa ajili ya mashabiki wake Unadhani ni Nini kitatokea hapo kati ya Rosa Ree na Awilo Longomba kama wakiamua kufanya ngoja ya pamoja?

SEX MACHINE - SEHEMU YA 05

Image
SEHEMU YA 05  Baada ya muda kidogo alinyanyuka na kuwasha gari yake hiyo, ila kabla ya kuliondoa, aliwasha redio na kuutafuta wimbo wa mwanamama Celine Dion. wimbo unaokwenda kwa jina la 'That the way It is'. ambao aliamini kidogo unaweza kuyapeperusha mawazo yake kwa muda huo.  "When you want it the most,  there's no easy way out,  when your heart's left in doubt" ndivyo alivyokuwa akiufuatisha wimbo huo huku akitingisha kichwa kidogo kidogo. Wimbo huo ulimfanya ayasahau mawazo lukuki yaliyokuwa kichwani mwake.  "When you question me for a simple answer,  i don't know what to say,  no but it's plain to see,  if we stick together. Your gonna find the way yeah." Kwakweli wimbo huo ulimpeleka mbali kihisia, ulimfariji kwa kiasi fulani hadi nyumbani kwake akapaona karibu sana. alifika nyumbani kwake bila matarajio. Alikibonyeza kitufe fulani kwenye rimoti na lango kubwa la jengo hilo likafunguka. lilikuwa ni jengo kubwa na la thamani kweli amba...

SEX MACHINE - SEHEMU YA 04

Image
SEHEMU YA 04  Hivi mnajua hii kazi ni ya kuchambua mchicha eenh! Inabidi muwe ngangari kwenye kampuni hii na sitawavumilia watu wazembe tena. Mtakufa." Ikamaliza sauti hiyo kwa kutoa kalipio baya sana kwa washirika wote wa humo ndani kisha mkoromo wa spika ukafuatia na kufuatiwa na ukimya kuashiria kuwa mkuu huyo alishakata mawasiliano. Minong'ono midogo midogo ikaibuka mahali hapo huku vijana maalumu wakihangaika na kuutoa mwili wa Mahmood eneo hilo. Joesan na Suzane wakaondoka na kuwaacha watu hao wakizidi kung'atana masikio na jambo likijadiliwa hapo ni namna Joesan atakavyoweza kumpata Sex Machine kwa muda huo mfupi ambao Suzane aliahidi. Kwao waliona ni jambo lisilowezekana na ni kama walijivalisha njuga na ilhali kucheza ngoma lilikuwa ni timbwili kubwa.  "Kwanini huyu binti anajipendekeza sana kwa Joesan?" aliuliza mzee mmoja wakiwa wawili baada ya kutoka kwenye ule ukumbi wa mikutano.  "Mgobo, Suzane ni lazima ampigie kifua Joesan, kwani yule ni ...

Lulu Ashindwa Kuvumilia kwa Alikiba

Image
Staa wa Bongo Muvi, Elizabeth Michael ‘Lulu’ ameshindwa kujizuia na kujikuta akipagawa na kuweka hisia zake wazi juu ya wimbo wa staa wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba ‘King Kiba’. Lulu amejikuta akipagawa na Wimbo wa Mshumaa wa Kiba baada ya kuona vijana wake wa Kundi la Kings Music wakiuimba wimbo huo laivu kwa kutumia gitaa. Lulu alitupia video fupi ya jamaa hao kwenye ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter ikiwaonesha Cheed na Tommy Flavour wa Kings Music wakiimba wimbo huo kisha aliandika; “Niko mahali kwenye ukuta wa chupingi, najikuna vipele vya baridi (goose bumps).” Hata hivyo, Lulu aliungwa mkono na staa mwenzake wa Bongo Muvi, Wema Isaac Sepetu ambapo naye kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa Instagram alionekana akiongea na Kiba kupitia video call ya Mtandao wa WhatsApp kisha akaandika; “Na mniache, asante kwa hii track.” Naye mwigizaji Esha Buheti aliandika; “Weee Ali (Kiba) sikuachii mpaka kufa.”

SEX MACHINE - SEHEMU YA 03

Image
SEHEMU YA 03  "Ni kweli Chriss nina makosa lakini siyo kwa hukumu hiyo, inamaana umeshindwa hata kujizuia my love...? No, i don't belive that Chriss umenikosea sana." Alilalamika sana Salome hakutegemea kutokea kwa jambo hilo kiwepesi namna hiyo. Chriss alimuangalia msichana huyo kwa kina na kisha akakifungua kinywa chake tena.  "Naomba unisikilize kwa umakini mkubwa we binti, ulishindwa kulifanya hili liwe siri baina yangu mimi na wewe ukaamua kumwambia kila kitu Maida. Ukitegemea kwa mtoto wa kike kama yeye angekwenda wapi kumalizia haja zake na ilhali mnajua mazingira mnayoishi? eenh...!"  "hata kama siyo kwa namna hiyo Chriss, mimi siyo wa kuchangia penzi na Maida." Salome alimkatisha Chriss na kusema maneno hayo kwa sauti ya juu sana tena alikuwa akiongea huku machozi yakianza kujichora machoni mwake.  "Hujui ulisemalo na laiti ungejua, ungekwisha kuufunga mdomo wako!" Alisema namna hiyo Chriss na kumfanya Salome kuganda kwa muda mithi...