Posts

Showing posts from January, 2020

RIWAYA:: MAISHA YANGU YA UVUVI SEHEMU YA THELATHINI NA TATU 33

Image
ENDELEA.......  Baada ya kumalizana na yule mganga alituruhusu huku akitupatia masharti ya kawaida sana ambayo kwa yeyote kati yetu angeweza kulitatua.  Mshana pamoja na mimi tulimhofia yule kiumbe ambae kwa mujibu wa mganga kuwa tayari kamkamata na hawezi kutoka tena mpaka pale atakapommaliza kabisa na apotelee mbali. Safari yetu ilikuwa yenye wasiwasi mkubwa sana lakini tulijitahidi kufika nyumbani salama bila hata kuwa na kipingamizi chochote. Mshana alizidi kunitia moyo kuwa nisijali kutokana na yale ambayo yanajitokeza.  Akili yangu ilibaki kuwaza familia yangu inaendeleaje huko iliko, ghafla gari linaingia pale tulipo na wanashuka Vijana wawili Manyota na Musa ambao moja kwa moja walikuja kunikamata bila hata kujua sababu ni nini zaidi. Walinilazimisha kufika hadi kwenye lile gari ambalo alikuwemo Mzee Paul pamoja na Salha.  Nilijua kuwa leo hii kazi ipo na lazima wanifanyie kitu mbaya watu hawa. Walinibeba hadi kufika kwenye nyumba ya moja ambayo sikuweza kuitambua vyema. Walini

RIWAYA: MAISHA YANGU YA UVUVI SEHEMU YA THELATHINI NA MBILI 32

Image
ENDELEA………………………  ……………Mshana alinilazimisha nikimbie baada ya kumueleza kuwa yule kiumbe anakuja kwa kasi ya ajabu sana. Ndipo niliungana nay eye kumfuata kule ambako anaelekea. Tulitumia nguvu nyingi sana katika kuhakikisha kuwa yule kiumbe hatukuti. Lakini cha ajabu Zaidi alikuwa ana hema karibu yangu hata kila ninapojaribu kuongeza spidi ni kama nakimbizana na chombo cha moto kama vile pikipiki ama gari maana nilizidi kuchoka mimi tu.                Tulipofika mbele Zaidi kulikuwa na njia pacha ambazo ziliweza kutuchanganya kwa kweli, ghafla tulisimama pale tukihangaika huku hatufahamu wapi tunaelekea, Mshana alinihoji kujua kama yule kiumbe anakuja ama laa!.  “Mnali vipi anakuja huyo kiumbe unamsikiaaa?”  Aliniuliza Mshana.  “Hapana simsikii kabisa kwa sasa ehee wapi tunaelekea?”  “Eheee huku hapa twende haraka”.  Tulisonga mbele lakini jambo ambalo lilinishangaa ni kwa kutosikia sauti ya yule kiumbe tena. Tuliendelea kukimbia hadi eneo Fulani lenye miti mingi sana alafu kupo na k

RIWAYA:: MAISHA YANGU YA UVUVI SEHEMU YA THELATHINI NA MOJA 31

Image
Endelea.......  .............Tulibaki kushangaana mule ndani hali kila mmoja ana maumivu yake. Kwa upande wa Mshana alichukia sana kuhusu kile kitendo kwa kuwa anafahamu nini kimefanyika.  Ghafla nje tunasikia watu wakikimbizana ovyo na wengine wakiwa wanalia moja kwa moja tulijua kuwa lile lijitu limeanza kuua watu. Kumbe haikuwa kama vile ambavyo tumefikilia ilikuwa ni tofauti kabisa.  Mimi na Mshana tulitoka taratiibu na kuelekea nje ili tukaangalie nini kimetokea.  "Mshana.."  "Eeeh!"  "Unajua tufanye nini hapa.."  "Nakusikiliza Mnali"  "Inabidi tufute kwanza mawazo ya kwenda kwa mganga kwanza tuwaze mengine kabisa alafu baadae inawezekama tukawaza hilo na tukaenda kabisa".  Alikubali wazo langu japo ni ngumu kuacha kuwaza jambo ambalo lipo kichwani mwa mtu alafu umuambie kuwa asijaribu kabisa kuwaza ni jambo la ajabu. Tulipotoka nje tukawaona watu kadhaa wanakimbia ndipo walipofika pale tulipo na kuanza kuhema kwa harakaharaka sana

RIWAYA:: MAISHA YANGU YA UVUVI SEHEMU YA THELATHINI 30

Image
ENDELEA.......  ................Nakumbuka ilikuwa siku ambayo nilipanga niende kuanza rasmi kazi ya uvuvi tena ili niweze kupata kiasi ambacho kitanisaidia kutafuta familia yangu. Lakini asubuhi hiyo wakati naelekea pwani niliwaona watu wakikimbilia maeneo hayo. Nilishikwa na mshangao ikabidi na mimi niwahi kujua kuna jambo gani. Nilipata kumuuliza mmoja wa wale wanaoelekea huko. Ndugu habari yako..Salama vipi?, eti huko kuna jambo gani mbona watu wengi wanakimbilia huko?. Haah! Ndugu kuna watu watatu wamekufa wamekutwa nchi kavi wamekufa ila kilichowauwa hakifahamiki. Mh nilishtuka sana. Tulifuatana njianibkuelekea huko. Ghafla ile sauti ya mngurumo karibu yangu ikanijia naisikia sana inanguruma, ilinichukiza sana na hadi ikanifanya safari yangu iwe nzito. Nilimuambia yule jamaa basi atangulie tu. "Ndugu basi wewe tangulia tu nitakukuta, vipi kuna shida, hapana ila nenda tu basi. Nilimuacha aende ili yasije kutokea mengine tena. Tulipofika kule kweli tuliwakuta polisi wakiwa wame

RIWAYA:: MAISHA YANGU YA UVUVI SEHEMU YA ISHIRINI NA NANE 28.

Image
ENDELEA............  .................Ndipo pale nilipoamua kuwaambia ukweli ili yasije kutokea mapema kabla hata niliyokwenda nayo pale hayajitimia. "Jamani naombeni mnisikilize, huku tunakoelekea si kuzuri kabisa, kwa maana kuwa kuna viumbe vya ajabu sana". Walinishangaa wakati yule mwingine alishafika tayari nchi kavu na mimi nikiwa na yule mwingine tupo ndani ya maji bado. "Kwa nini unasema hivyo na viumbe gani hao wa ajabu ambao wanaweza kututishia sisi maisha". Niliona vyema kuwaeleza kwa kutumia busara kubwa ambayo ingeweza kunifanikishia mimi yale malengo yangu muhimu. "Huku kuna viumbe vya hatari sana, viumbe ambavyo vinapenda kukaa nchi kavu pekee, lakini ndani ya maji hawawezi kabisa kukanyaga". "Kwa hiyo?". Aliuliza mmoja wao. "Inachobidi tulale ndani ya maji mpaka asubuhi au laa tukae ndani ya maji hadi asubuhi ndipo tutaanza kutoka na kuwapeleka huko ambako mnataka." Walishtuka lakini ndipo wakaanza kuongea wao wenyewe. &#

Simulizi - Mambo ya wikiend bhanaaa

Image
Ilikuwa ijumaa ya wiki,  watumishi wa umma na sisi wa sekta binafsi sote  tumejidamka zetu makazini kama kawa, si unajua tena… mambo ya  kuwajibika. Mambo yote yamekwenda sawa, ila tu kwa kutimiza wajibu wangu mwingine usio rasmi, nachelea kuwadokolea kidogo yaliyojiri. Ni stori inayomhusu Dada Jesca, mhazini wetu pale ofisini. Kisa kilianza kwa kuwa aliwahi kutoka kazini kuliko ilivyo kawaida yake, na kama ilivyo ada ya kamera yetu ya simulizi kutoka jikoni ikamfuatilia kujua kulikoni ?!! Si unajua tena… Basi siku ile, kwanza Dada Jesca alikuja akiwa ameupara na kupendeza kwelikweli ingawa kwa kweli maumbile ya mtoto wa kike huyu hata akivaa maturubai anavutia, pili aliomba ruhusa mapema sana aweze kurudi nyumbani kwa kuvunga kuwa eti anajisika vibaya, mmh… kumbe mumewe alikuwa yu njiani kurudi toka safari ya wiki tatu na alikuwa ana hamu naye kupita maelezo. Tukumbuke kuwa ni miezi miwili tu imepita tangu Dada Jesca alipofunga pingu za maisha na kijana Badi na kuanza naye

Athari 10 za wivu katika Mapenzi, mahusiano au ndoa

Image
Ikiwa unafikiria wivu si kitu, fikiria tena! Kila mtu anajua kuhusu wivu, sawa? Labda umesoma madai kuwa wivu "mdogo" ni mzuri kwa mahusiano yako ya mapenzi au ndoa, au kwamba wakati mpenzi wako ana wivu, inamaanisha kwamba anajali sana. Ikiwa unapigana na wivu, labda unajua jinsi unavyoumiza na kuharibu mahusiano. Wivu sio mzuri kwa mahusiano yako, na sio mzuri kwako pia. Ingawa mwenye wivu hutambua kuwa wivu huo hauna manufaa, lakini ni moja ya vitu ambavyo bado huwezi kuacha kirahisi Umeweza kujaribu jaribu njia zako binafsi za kuacha wivu. Pengine umejaribu kwa bidii kufuta mawazo ya wivu ambayo yanaingia ndani ya akili yako na kisha kujenga na kukusababisha kusema au kufanya mambo unayojuta baadaye. Lakini ... Bado unaupata kiurahisi sana. Bado unamhoji mpenzi wako, au unajilinganisha na wengine kwa wasiwasi kwamba utasalitiwa na mwenza wako. Wakati mwingine unapopatwa na vita kati yako na tabia mbaya kama wivu, fikiria madhara yanayoweza kutokea. Angalia mambo ambayo ta

SIRI YA KASI YA MBEGU ZA KIUME YAGUNDULIWA!

Image
Wataalamu wanasema wamegundua kwamba mbegu za kiume huanza kwenda kwa kasi wakati zinapofika karibu na yai la mwanamke, suala ambalo huenda siku zijazo likasaidia katika kupatikana dawa ya kuzuia mimba ya wanaume. Vitundu vidogo vilivyoko juu ya mbegu hizo za kiume huziwezesha kubadilisha PH yake ya ndani, ambayo hufanya mkia wa mbegu hizo uanze harakati. Wataalamu hao wa Chuo Kikuu cha California huko San Francisco wanasema kuwa, ugunduzi huo unaweza pia kusaidia kuelezea kwa nini marijuana huwafanya wanaume wawe tasa na kwamba suala hilo litaleta mabadiliko makubwa katika kufahau suala zima la uwezo wa kuzaa wa mwanaume. Kwa kawaida mbegu za wanaume hazianzi kwenda mbio baada tu ya kumwagwa, na ili kuweza kulifikia yai la mwanamke huhitajia kujiepusha na kasi hadi pale zinapokaribia yai. Wanasayansi kwa muda mrefu wamekuwa wakifahamu kwamba mwendo wa mbegu za kiume umekuwa ukisimamiwa na PH ya ndani, na kuwa kwake katika hali ya asidi au alikali lakini walikuwa hawafahamu ni jambo g

RIWAYA:: MAISHA YANGU YA UVUVI SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA 27

Image
ENDELEA.......  .  ..  ...  ....  .....  ......Baada ya kuhakikisha kuwa nimeitupa ile simu hapo ndipo shughuli mpya ilipoanza. Mguu wangu uliniuma sana mpaka kiuno kikawa kinanibana kisawasawa. Ilifikia hali kuwa hata natamani yale maeneo yakatwe nibaki na kidonda kipya ambacho kinaweza kutibika kuliko hii hali.  Nilikaa takribani masaa kadhaa ambayo yalinifanya niwaze kuwa wale watu hawawezi kurudi tena. Kutokana na hilo nilijikokota na kusimama taratibu ili niangaze kule ambako waliingilia. Nilihisi kuwa ndio wamenitelekeza pale au vijana wa mjini wanasema wameniacha mataa. jambo kubwa zaidi ni wao kutowamini hali ya kutowafahamu. Muda ulivyozidi kusonga ndipo hali yangu na mimi ilizidi kuniwia ngumu sana. Lakini nilijikaza ili nifikie lengo langu. Maisha yangu yamekuwa magumu pia yenye kupitia misukosuko ya kila siku tangu nimeanza hadi sasa, na sijui lini nitapata faraja ambayo itanifanya nijihisi huru kama pale awali.  Kwa mbali ndipo nililiona gari likija yale maeneo nilijikokot

Mwanamke;Mwanaume Anapokuambia Hakutaki Tambua Mara nyingi huwa wanamaanisha kweli

Image
Hakuna cha labda atabadilika, labda ana hasira, labda flani kamuwekea dawa, labda marafiki zake ndiyo wanamdanganya, labda nikwasababu niko hivi, labda nikwasbabu niko vile, labda nikwasababu hajanijua vizuri au sababu nyingine yoyote ile ambayo unaitumia kujipa moyo. Wanaume wameumbwa tofauti na wanawake, wakati mwanamke anaweza kusema sitaki akimaanisha kuwa anataka ila tu uongeze nguvu katika kumbembeleza na kuongeza vishawishi, mwanaume anaposema sitaki, sikutaki anamaanisha hataki, sikutaki. “ Kuna wanawake wengi wapo kwenye mahusiano ya labda atabadilika, wapo na wanaume ambao wameshawaambia kua hawatawaoa au hawana mipango ya baadaye nao lakini bado wana ng’ang’ania wakidhani kuwa watabadilika. Nikweli wanaweza kubadilika lakini mara nyingi huwa ni kwa muda, watakuwa na wewe kwa muda hata kwenye ndoa lakini ipo siku kile kilichowafanya wakuambie kua sikutaki kitaibuka na utaishia kuumia. Kwa kawaida wanaume wanakuwa wawazi na humaanisha kile wanachokisema. Hapa naomba mnielewe k

Ukiamua Kuwa na Mahusiano na Mume wa Mtu Lazima Ukubali Kuwa Mtumwa wa Mambo Yafuatayo

Image
Ukiamua Kuwa na Mahusiano na Mume wa Mtu Lazima Ukubali Kuwa Mtumwa wa Mambo Yafuatayo: 1. Baby samahani dakika moja,wife anapiga simu 2. Baby muda umeenda Sana mke wangu atanipigia, wacha niwahi kurudi nyumbani, Kesho saa 12 nitakuwa hapa 3. Bby nataka kuja kulala kwako mke Wangu amefiwa kaenda kwao 4. Baby sintaweza kuja Leo, wife kanibana… Pole kwa kuugua 5. Baby tangulia mbele, nitakukuta… Pale wanakaa shemeji zangu, wakituona pamoja watamuambia wife 6. Unaweza kimbiwa katikati ya sherehe usipewe hata nauli ya bodaboda, kesho unaambiwa sorry darling, si uliona wife alitokea ghafa 7. Mkiwa mnaongea kwa simu kwa mahaba mara unashtukia unaitwa Hamadi na kuagwa fasta.,baadae unaambiwa mke wangu alitokea ghafla nikawa sina jinsi 8. Unaweza pitwa barabarani na mvua inanyesha,kesho ukaambiwa nilikuona my love, Ila ningefanya nini.. ,nilikua na mke wangu Ili mwisho wa siku ukija kupewa mimba na kuterekezwa usije na kauli zako za kusema wanaume wote ni mbwa na kama utafikia hatua ya kuwaita

Vanessa Mdee Aendelea Kumpa Sifa Mpenzi Wake Rotimi….

Image
Vanessa Mdee afunguka vigezo vya mwanaume wa kuwa mumewe baba watoto wake, mojawapo ni kuwa na mapenzi ya kweli – – “Siku zote nimekuwa nikitamani kuwa na mwanaume mwenye roho nzuri, sio yule ambaye akiwa na mimi anani- treat vizuri lakini akitoka huko nje anakuwa na roho mbaya, lakini pia awe na akili na mcha Mungu kwa sababu mwanaume akiwa na hofu ya Mungu anakuwa na heshima kwa wanawake, mpenzi wangu(Rotimi) anavyo vigezo hivyo, tuzidi kuombeana,” Vanessa ameiambia GPL

Kobe Bryant Kutunukiwa TUZO ya Heshima ya Oscar…..

Image
Wakati dunia ikiwa bado katika simanzi nzito ya kuondokewa na nguli kwenye mchezo wa Basketball Kobe Bryant, waandaaji wa Tuzo za Oscar wametoa taarifa kuwa watampatia tuzo ya heshima Kobe Bryant kutokana na mchango wake katika jamii, tuzo ambazo zinategemewa kufanyika February mwaka huu 2020. Mara ya mwisho Kobe Bryant kupata tuzo hiyo ilikuwa ni mwaka 2018.

Mpangaji Mwenzangu Ananitega Kila Akiniona Ananigeuzua Wezele Lake

Image
Huyu ni mpangaji mwenzangu, ameolewa nami nina mke, kwa siku kadhaa mke wangu ambae nampenda sana yuko likizo hivo kila nikurudi au napokuwa nafanyafanya vishughuli vya hapa nyumbani huchukua nguo na kuanza kufua huku akiwa ameelekeza kwangu wowo lake kama inavoonekana kwenye picha hii.  Sasa naombeni ushauri maana nahisi mwaka huu mpya sitaweza kuvumilia huu ujinga, lakini kabla ya yote naomba ushauri

Ujue Msitu wa Ajabu Japan Ambapo Maelfu ya Watu Wamekufa Kimiujiza

Image
Aokigahara au msitu wa kujiua au bahari ya miti ni msitu ambao una ukubwa wa 35 square- kilomita ambao uko karibu na milima ya fuji huko japan msitu huu ni msitu ambao mbali ya kuwa ni kivutio kikubwa cha watalii ni msitu ambao unasemekana kuwa una mambo ya ajabu, kutisha na kuogofya ni kawaida kabisa ukiwa ndani ya msitu wa Aokigahara ukisikia unaitwa jina lako na mtu asiyeonekana iwapo ukiwa ndani ya msitu huo. pia inasemekana kuwa unaweza kumuona mtu kwa mbali kwenye miti ya msitu huo ukifuatilia huoni mtu kwa maana watu hao wanapotelea kwenye miti Msitu huo unasemekana una mapepo ya kujapan kwani tokea uwepo wake ni maelfu ya watu wamekuwa wakikutwa wamekufa maeneo hayo haya kwa kujiua ambapo kwa mwaka 2010 pekee watu 54 wamekutwa wamekufa ndani ya msitu huo tafiti zaidi zinasema kuwa tokea mwaka 1988 walipoanza kufanya hesabu za watu wanaojiua msituni hapo ni watu 30 kila mwaka huenda msituni hapo na kujiua In 2003, miili 105 ilikutwa msituni watu wakiwa wamejiua, ambapo iliizidi

Kwenye Hili, Wolper Adai Kutangaza vyema Taifa

Image
Msanii wa filamu nchini Jacqueline Wolper, amesema siku atakayopagawa ndiyo atam post mpenzi wake pia yeye ni mmoja wa watu ambao wanalitangaza vyema Taifa kwa kuwa na mpenzi nje ya Nchi. Akipiga stori na EATV & EA Radio Digital, Jacqueline Wolper amekiri ni kweli ana mpenzi mpya nje ya nchi, huwa anawasiliana naye mara kwa mara na akimkumbuka huwa anamfuata huko alipo. “Mnataka hadi muone tunapost wapenzi wetu ndiyo mjue kama yupo, sasa hivi nipo huru sana naona kama nimezaliwa upya yaani, nimebadilika sana ila siku nitakayopagawa nitampost bado sijapagawa na sijataka, mpenzi ni ninaye na tunawasiliana, unadhani nitakaaje sasa kwa kuwa yeye yupo mbali na hatuishi pamoja wala nchi moja” ameeleza Jacqueline Wolper. Aidha Jacqueline Wolper ameongeza kusema “Kutoishi naye pamoja kunafanya mara chache sana kuwa kimapenzi na sasa hivi nipo kikazi zaidi, nikimkumbuka nitaenda kumfuata au yeye atakuja naitangaza vizuri sana nchi”.

RIWAYA:: MAISHA YANGU YA UVUVI SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA 26

Image
......  .................Ule uharaka wa lile gari ulinifanya niweweseke na bila hata kutambua kinachoendelea. Mlinzi ambae alikuwa kwenye nyumba ile ya salha alishtuka kwa haraka sana akataka kufungua mlango ajue nini kinaendelea.  Lakini alitokea jamaa mmoja ambae sikuweza kumfahamu vyema kutoka kwenye lile gari lake na kuninyanyua fasta kwa haraka sana hadi kwenye gari na kufunga mlango na yeye kuingia upande wake. Nikiwa mule ndani nilifungwa pingu mikononi hadi miguuni pia jamaa yule maana walikuwa wawili wakanifunga mdomo, safari ya gari lilikwenda huku nikizidi kutapatapa maumivu ya mguu wangu, pia sikuwa nafahamu wale akina nani, safari iliiva hadi ufukweni kabisa wa bahari ndipo waliponishusha.  Nilikuwa nachechemea kutokana na mguu wangu kuharibika sana. Yule dereva alifungua mask yake usoni na nikapata kumuona sura yake ila kadri nilivyojitahidi kuvuta taswira ilizidi kukataa kutokana sikuwa namfahamu kabisa.  "Kijana samahani kwanza kwa hili tendo ambalo tumekufanyia mu

RIWAYA:: MAISHA YANGU YA UVUVI SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO 25

Image
ENDELEA............  .................  ................  Basi ndipo Salha akaingia ndani ya gari kisha akafunga mlango wa gari yake na kuondoka yale maeneo. Nikiwa nazidi kuwaza hali yangu ya maisha niliyonayo ndipo nikagundua kuwa hata matajiri hawana furaha kwa hali hii. Kama mimi mwenye maisha magumu naishi kwa raha lakini kwa hatua chache ya kushuhudia maish ya wale walioendelea naona kabisa wanapata tabu.  Gari lilifika hadi kwenye nyumba yake na mlinzi akafungua geti haraka sana na sisi tukapata kuingia. Akili ya Salha ililala sana kwenye mapenzi tofauti na mimi mawazo yangu aliniangalia kwa jicho la mahaba lakini mimi nilimkata jicho tu. Sikutaka kumuonyeshea moja kwa moja kuwa nimemkubalia ndio maana nilikaza baadhi ya sehemu kama hizo ambazo yeye alizifanya.  Alinishika mkono tukaelekea ndani baada ya kufungua mlango wake. Nilifika nikatulia kwenye kochi pale sebuleni kisha nikajishika kichwa changu huku nikitazama jinsi Mzungu alivyotengeneza taa na ikawa inatoa mwanga mzuri